Monday, October 8, 2012

MOURINHO: KUMLINGANISHA RONALDO NA MESSI SASA NI MARUFUKU

















KOCHA wa Real Madrid, Jose Mourinho amewasifu Cristiano Ronaldo na nyota wa Barcelona, Lionel Messi baada ya wawili hao kufunga mara mbili kila mmoja katika sare ya 2-2 juzi usiku na ametaka ipigwe marufuku kuwalinganisha. 

Alipoulizwa nani anapaswa kutwaa tuzo ya Ballon d'Or ya mwanasoka bora wa dunia, alisema: "Sitaki kuiwaza sana hiyo. 

"Nadhani ipigwe marufuku sasa kusema nani ni mwanasoka bora wa dunia kwa sababu hawa wawili ni wa sayari nyingine. 

"Ningependa mchezaji wangu ashinde kwa sababu yeye ni bingwa wa ligi bora duniani, lakini nadhani wote ni wachezaji wazuri sana."

No comments:

Post a Comment