Wednesday, October 10, 2012

STAILI YA UNYOAJI NYWELE YA RONALDO YAWEKWA WAZI NA KINYOZI WAKE
 

Vinyozi wa Cristiano Ronaldo, Jose Miguel na Siero Leal

CRISTIANO Ronaldo alimshangaza kila mmoja kwenye Uwanja wa Nou Camp Jumapili kutokana na mwonekano mpya. Ilikuwa ni staili ya nywele iliyoonyesha alama ya V. Wakati alipofunga goli la kwanza alionyesha kidole chake kwenye alama ya ushindi kichwani mwake. Kuna stori nyuma ya staili hiyo.

Mreno huyo aliwapa vinyozi ambao ni ndugu Jose Miguel na Siero Leal. Aliwaita Jumamosi na kuwaeleza kwamba anatafuta staili mpya, kitu tofauti na kitakachozua mjadala.

"Alituambia, kama ilivyo mara nyingi kwake, anahitaji kitu tofauti. Tunamfahamu vyema na tukapata wazo la kumnyoa kwa alama ambayo inamaanisha amani na utulivu ambao huupata shujaa baada ya mapambano. Alikubali," alisema mmoja wa vinyozi hao.

Kuifanya ionekane kitu kizuri ilikuwa ni jambo jepesi. Jose alisema: "Sio tu staili. Kuna sababu katika kila staili ya kunyoa. Na anahitaji staili inayoonekana. Inamfaa. Yeye ni mwenye malengo na anayependa vitu bora. Tulifanya alimbunia kilichokuwa katika hisia zake kwa wakati ule na kilionekana wakati wa mechi".

"Nywele zake ni laini sana na unapaswa kuzinyoa kwa umakini. Anapenda kuziseti ama kuzipaka mafuta mengi. Anafahamu kwamba kamera za televisheni humfuatilia kwa kila afanyalo na anapenda kuonekana mtanashati. Cristiano anajioenda sana na anapenda kutimiza malengo. Ni mshindi. Anajifikiria yeye tu," aliongeza.

No comments:

Post a Comment