JOSE MOURINHO: BALOTELLI NI KAMA KICHAA...NAWEZA KUTOA KITABU CHA KURASA 200 KUELEZEA VITUKO VYAKE NILIPOKUWA KOCHA WAKE INTERMILAN

 

 
MADRID, Hispania
Kocha wa Real 
Madrid, Jose Mourinho amezungumzia kipindi chake cha kuwa na straika 
Mario Balotelli wa Manchester City wakati akiifundisha Inter Milan na 
kusema kwamba mchezaji huyo ni kichaa.
Mourinho ameongeza kuwa akitaka, anaweza kuandaa kitabu kitakachoongoza kwa mauzo kuhusiana na migongano yake na Balotelli.
“Naweza
 kaundika kitabu cha kurasa 200 kuelezea mikwaruzano yangu na Mario 
wakati wa kipindi changu cha miaka miwili nikiwa na Inter Milan, lakini 
kitabu chenyewe hakitakuwa cha simulizi – kitakuwa ni cha vidhekesho,” 
amesema Mourinho.
“Nakumbuka kipindi fulani tulipokwenda kucheza 
dhidi ya Kazan katika Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya. Katika mechi hiyo 
mastraika wangu wote walikuwa majeruhi. Sikuwa na Diego Milito, wala 
Samuel Eto’o, nilikuwa na wakati mgumu hasa na Mario ndiye aliyekuwa 
mchezaji pekee wa nafasi hiyo.
“Mario akapata kadi ya njano 
katika dakika ya 42, kwa hiyo wakati tulipokuwa kwenye chumba cha 
kuvalia katika kipindi cha mapumziko nilitumia takriban dakika 14 kati 
ya 15 zilizopo kuzungumza na Mario tu.
“Nilimwambia: ‘Mario, 
siwezi kukutoa, sina mastraika wengine katika benchi, kwahiyo usimguse 
mtu na badala yake cheza mpira tu. Tukipoteza mpira, we usifanye lolote.
 Kama mtu akikuchokoza, we tulia, kama refa akikosea, we achia tu.'
 
No comments:
Post a Comment