| Sheikh Ponda Issa Ponda, akifunguliwa 
pingu, baada ya kufikishwa kwenye chumba cha mahakama ya hakimu mkazi 
Kisutu jijini Dar es Salaam jana Alhamisi Novemba 1, 2012. Kiongozi huyo
 mwenye msimamo mkali, alifikishwa kwa mara ya pili jana pamoja na 
wafuasi wake ambapo hakimu anayesikiliza kesi dhidi yake, Victoria 
Nongwa, ya kuvamia eneo la Markaz, Chang'ombe jijini Dar es Salaam, 
ambapo waliharibu  na kuiba mali vyote vikiwa na thamani ya shilingi 
milioni 59, madai ambayo washtakiwa wote waliyakanusha. Hakimu huyo 
alikubali kutoa dhamana kwa washtakiwa wote isipokuwa kiongozi huyo 
ambaye ni mshtakiwa namba 1 kwa madai kuwa bado Mkurugenzi was Mashtaka 
nchini (DPP), hajaondoa pingamizi lake la kuzuia dhamana kwa mshtakiwa 
namba moja. Ulinzi katika mahakama hiyo haujawahi kutokea katika miaka 
ya hivi karibuni, ambapo pamoja na mambo mengine, palifungwa CCTV 
Cameras, vifaa vya kugundua vitu vyenye asili ya chuma, polisi wa 
kutuliza gharsia magereza na wale wa FFU, polisi wa farasi na mbwa, 
pamoja na askari kanzu waliotapakaa kila kona ya maeneo jirani na 
mahakama hiyo kubwa jijini Dar es Salaam. Kikundi kidogo cha wafuasi wa 
ssheikh Ponda, kilijaribu kuleta rabsha, lakini polisi walitumia busara 
na kuwaelekeza kilichoamuliwa mahakamani ambapo pamoja na kusuasua 
kuondoka eneo hilo la mahakama, lakini hatimaye waliondoka huku  polisi 
wa kutuliza ghasia wakiwafuata kwa nyuma hadi eneo la makutano ya 
barabara za Bibi Titi na ile ya Morogoro nao wakatawanyika. Kwa mujibu 
wa vyanzo vya uhakika vya habari, kulikuwepo taarifa kuwa wafuasi hao 
walipanga kutega milipuko kwenye eneo la mahakama na pia walisambaza 
vipeperushi vyenye vitisho kadhaa, ikiwa ni pamoja na kufanbya 
maandamano makubwa ya kulazimisha kiongozi huyo aachiliwe. Kesi hiyo 
iliahirishwa hadi Novemba 15 mwaka huu itakapotajwa tena | 
No comments:
Post a Comment